KIPIMO CHA VYOMBO VYA HABARI
BARANI AFRIKA
Tanzania 2019
Muhtasari
Mwaka 2015, Tanzania ilifanya uchaguzi mkuu ambao ulimweka madarakani
Rais wa sasa Mheshimiwa John Pombe Magufuli. Kwa muda mfupi, Rais
Magufuli alikubalika na wengi kutokana na jitihada zake za kupambana na
rushwa ambazo zimesababisha maofisa wengi wa serikali kutolewa katika nafasi
zao. Utawala huu mpya pia umechukua hatua madhubuti kuongeza nidhamu
katika utumishi wa umma. Hata hivyo, mtindo wa utawala wa Rais Magufuli
na hasa kuhusu uhuru wa kujieleza na uhuru wa habari umekuwa chanzo cha
madhila makubwa. Kwa kiasi kikubwa, amejiimarisha kiutawala na kuhodhi
maamuzi ili kujijengea umaarufu; vyama vya siasa vya upinzani vimeminywa,
wakosoaji wa serikali wamekuwa wakikamatwa, na haki ya msingi ya uhuru
wa kujieleza imeathirika vibaya. Mambo haya yanayoogofya ni sehemu tu ya
mabadiliko katika nyanja nyingi nchini Tanzania katika kipindi cha miaka minne
iliyopita.
Ingawa Tanzania ina katiba ambayo imeeleza haki za msingi za kiraia na za
kisiasa, ikiwa ni pamoja na uhuru wa kukusanyika na uhuru wa kujieleza, haki
hizi zimeminywa. Katika kipindi cha miaka mitatu tangu mwaka 2015, sheria
kadha wa kadha za vyombo vya habari zilipitishwa, ikiwemo Sheria ya Vyombo
vya Habari ya mwaka 2016, ambayo ina mianya na madhaifu mengi yanayominya
uhuru wa kujieleza. Sheria hii inaipa serikali mamlaka makubwa juu ya maudhui
ya habari na utoaji leseni kwa vyombo vya habari na waandishi wa habari. Sheria
hii pia inaweka adhabu kali, ikiwemo kifungo gerezani, endapo chombo cha
habari kitachapisha habari za kuikashfu serikali, uchochezi, au maudhui mengine
yasiyozingatia sheria.
Wakati wanajopo wakiendelea na mjadala, mabadiliko ya hivi karibuni ya Sheria
ya Takwimu ya Mwaka 2015 yanamtaka mtu yeyote au taasisi kupata idhini ya
Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) kabla ya kutoa takwimu kwa matumizi ya umma.
Sheria hii ilibadilishwa katika kipindi cha nusu mwaka wa 2019 na kwa hivyo
haizuii tena kuchapisha taarifa ya kitakwimu bila kupata ishini ya ya serikali,
lakini bado takwimu rasmi zimeendelea kuhitaji kibali cha NBS. Mnamo mwezi
Machi, kabla ya mabadiliko ya hivi karibuni, sheria hii ilitumika kufungia gazeti
linalomilikiwa na mtu binafsi la The Citizen kwa madai kwamba lilichapisha
taarifa za uongo, zenye kupotosha na za kichochezi. Gazeti hilo lilichapisha
habari kuhusu kushuka thamani kwa shilingi ya kitanzania (TZS) dhidi ya Dola
ya Kimarekani (US$).
Mnamo mwezi Machi 2018, serikali iliweka Kanuni za Mawasiliano ya Kielektroniki
na Posta (mtandaoni), ambao uliwataka wamiliki wa blogu na waendeshaji wa

6

KIPIMO CHA VYOMBO VYA HABARI BARANI AFRIKA TANZANIA 2019

Select target paragraph3