ENEO LA 4

4.6 Waandishi na wahariri wote hawajichuji
Kwa mujibu wa wanajopo, mtindo wa makala na taarifa ya habari umebadilika
miaka mingi kadri waandishi wa habari wanavyotambua uwezekano wa
kisasi kutokana na kazi zao. Baada ya kufungiwa mara mbili, wanajopo
walisema kwamba waliona mabadiliko ya mtindo wa kampuni ya Mwananchi
Communications, ambayo huchapisha gazeti la The Citizen na gazeti dada
linalotumia lugha ya Kiswahili la Mwananchi, ambalo linasifika kwa kuandika
taarifa makini. Kujichuja kumekithiri. ‘Kuna habari ambazo sitazisogelea kwa
namna yoyote ile,’ alisema mwandishi mmoja wa habari kwenye jopo. ‘Baadhi
ya watu wametoweka.’

Alama:
Alama za mshiriki mmoja mmoja:
1

Nchi inakidhi kiashiria

2

Nchi inakidhi vipengele vichache tu vya kiashiria

3

Nchi inakidhi vipengele kadhaa vya kiashiria

4

Nchi inakidhi vipengele vingi vya kiashiria

5

Nchi inakidhi vipengele vyote vya kiashiria

Wastani wa alama:
Alama ya miaka iliyopita:

✓

✓

✓

✓

✓

✓
✓✓

✓

✓✓

✓

1.8
2006: 2.1; 2008: 2; 2010: 1.5; 2012: 1.8; 2015: 2.3

4.7 Waandishi wa habari wana vyuo vinavyotoa
mafunzo rasmi pamoja na fursa ya kuinua
viwango vyao
Kuna fursa nyingi za mafunzo ya uandishi wa habari Tanzania. Baadhi ya vyuo
vikuu vinavyotoa mafunzo ya uandishi wa habari ni pamoja na : Chuo Kikuu
cha Dar es Salaam, Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine Tanzania, Chuo Kikuu
cha Tumaini (Dar es Salaam na Iringa), Chuo Kikuu cha Kiislam Morogoro na
Chuo Kikuu Huria cha Tanzania. Mbali na vyuo vikuu, idadi kubwa ya vyuo
vinatoa mafunzo ya uandishi wa habari kwa ngazi ya Stashahada na cheti. Hata
hivyo, wanajopo walisema kwamba ubora wa mafunzo wanayopata wanafunzi
unahitaji kuboreshwa. Ilielezwa kwamba wahadhiri wengi wa vyuo vikuu
hawajawahi kufanya kazi ya uandishi wa habari na hivyo hawana uzoefu katika
kuandika habari na kutafuta habari.
Fursa nyingine zinapatikana nje ya mfumo wa elimu. Daily News, ambalo ni gazeti
linalomilikiwa na serikali, mara nyingi huwapeleka waandishi wa habari nchini
China, shukrani kwa ubia na serikali ya China. Mashirika kama vile UNESCO
yamekuwa yakijihusisha na mafunzo na kuwezesha redio za kijamii na yamejenga
ushirikiano na na vyuo vya uandishi wa habari kutengeneza mfumo wa kujifunza
kielektroniki. Washiriki wengine wakuu ni pamoja na BBC Media Action, ambayo

53

KIPIMO CHA VYOMBO VYA HABARI BARANI AFRIKA TANZANIA 2019

Select target paragraph3