ENEO LA 4

4.5 Waandishi wa Habari na vyombo vya habari wana
uadilifu na si wala rushwa
Uhandishi wa habari wa bahasha ya kahawia, mtindo ambapo waandishi wa
habari wanapewa fedha taslimu na vitu vingine vya mkononi ili waipambe taarifa,
umeenea sana Tanzania. Kutokana na malipo kiduchu na mazingira mabaya
ya utendaji kazi, washiriki walisema kwamba waandishi wa habari walikuwa
kwenye hatari ya kupokea rushwa na mara nyingi walipata hisani ya vyanzo vya
habari na wenyeji wa matukio. Tabia hii imekithiri wakati wa chaguzi ambapo
viongozi wa kisiasa wanadaiwa kuwahonga waandishi wa habari ili kutangaza
kampeni zao.
Wanajopo walielezea aina ndogondogo za rushwa kama vile kukubali kupewa
usafiri, kulipiwa hoteli na zawadi nyingine zisizohusisha fedha na kubadilishana
na habari. Maslahi mahsusi ya mmiliki wa chombo cha habari pia yanaathiri jinsi
ya kutangaza habari.
Wanajopo walisema kwamba wafanyabiashara fulani wasingeweza kuandikwa
vibaya kwenye baadhi ya vyombo vya habari kutokana na ukaribu wao na
wamiliki wa vyombo vya habari.
Ni vigumu kumpata mwandishi wa habari atakayeandika kuhusu kashfa
inayomhusisha mtoaji mkubwa wa matangazo ya biashara. Kulikuwa na
mashtaka mahakamani kuhusu kampuni ya bia kutokana na kuzalisha
bidhaa mbovu. Kila wakati chumba cha mahakama kilikuwa kimejaa
waandishi wa habari, lakini hakuna habari yoyote iliyoandikwa au
kutangazwa baada ya hapo. Vyombo vya habari havitatangaza ajali
inayohusisha kampuni fulani za usafirishaji. Watoaji wakubwa wa
matangazo ya biashara wana namna yao ya kuvinyamazisha vyombo vya
habari.
Mashirika machache yana sera inayowataka waandishi wa habari kusema
zawadi na mambo mengine wanayopewa na watoa habari. ‘Lakini mara nyingi
watasema tu, “Acha hili liwe siri yetu,”’ alisema mmoja wa washiriki.

Alama:
Alama za mshiriki mmoja mmoja:
1

Nchi inakidhi kiashiria

2

Nchi inakidhi vipengele vichache tu vya kiashiria

3

Nchi inakidhi vipengele kadhaa vya kiashiria

4

Nchi inakidhi vipengele vingi vya kiashiria

5

Nchi inakidhi vipengele vyote vya kiashiria

Wastani wa alama:
Alama ya miaka iliyopita:

52

✓✓✓✓✓

✓

✓
✓

✓✓
✓

1.9
2006: n/a; 2008: n/a; 2010: 2; 2012: 1.5; 2015: 2.3

KIPIMO CHA VYOMBO VYA HABARI BARANI AFRIKA TANZANIA 2019

✓

Select target paragraph3