ENEO LA 4

4.4 Waandishi wa habari na wanahabari wengine
wamejiunga kwenye vyama vya wafanyakazi na/
au vikundi vya kitaaluma, ambavyo vinawakilisha
maslahi yao kikamilifu
Umoja wa Waandishi wa Habari Tanzania haujafanya kazi tangu mwaka 2011
lakini umoja mpya, ambao ni Umoja wa Wafanyakazi Waandishi wa Habari
Tanzania, ulikuwa ndo kwanza umeanzishwa. Pamoja na hilo, kuna Chama
cha Waandishi wa Habari za Maendeleo Tanzania, ambacho ni muungano wa
redio 35 za kijamii, ambacho kinapigania haki za waandishi wa habari wa redio
za kijamii kama sehemu ya malengo yake. Vyama vya wafanyakazi Tanzania
vimekuwa dhaifu. Kwa hivyo, vyama vya waandishi wahabari vina tabia ya
kuangalia mambo mengine yanayohusu vyombo vya habari kama vile haki za
vyombo vya habari, uhuru wa kujieleza na viwango vya kitaaluma. Kundi hili
linajumuisha Muungano wa Klabu za Wanahabari Tanzania, Jukwaa la Wahariri
Tanzania, Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania (TAMWA),
Chama cha Waandishi wa habari za Michezo Tanzania, Taasisi ya Vyombo vya
Habari Tanzania, Baraza la Vyombo vya Habari Tanzania na Taasisi ya Vyombo
vya Habari Kusini mwa Afrika. Washiriki walisema kwamba baadhi ya vyama
hutoza ada kubwa ya uanachama ambayo huwakatisha tamaa waandishi wa
habari wachanga. Hata hivyo, vyama hivi vimekuwa na nguvu katika kuwakilisha
maslahi ya waandishi wa habari. TAMWA inadhaniwa kuwa mojawapo ya vyama
vya waandishi wa habari vyenye ushawishi zaidi na mara nyingi hutajwa kama
taasisi ya kuigwa.

Alama:
Alama za mshiriki mmoja mmoja:
1

Nchi inakidhi kiashiria

2

Nchi inakidhi vipengele vichache tu vya kiashiria

3

Nchi inakidhi vipengele kadhaa vya kiashiria

4

Nchi inakidhi vipengele vingi vya kiashiria

5

Nchi inakidhi vipengele vyote vya kiashiria

Wastani wa alama:
Alama ya miaka iliyopita:

51

✓✓
✓

✓

✓✓✓
✓

✓
✓

✓

2.3
2006: 2.2; 2008: 2.3; 2010: 2.2; 2012: 2.3; 2015: 2.5

KIPIMO CHA VYOMBO VYA HABARI BARANI AFRIKA TANZANIA 2019

✓

Select target paragraph3