ENEO LA 3

inakipa chombo hiki wajibu wa kuutangazia umma na uhuru wa uhariri. Inaeleza
kwamba:
Kwa kuzingatia vipengele vya Sheria ya Mamlaka ya Mawasiliano
Tanzania, kutakuwa na Mkataba kati ya Shirika la Utangazaji Tanzania na
Waziri ili kuliwezesha Shirika la Utangazaji Tanzania kuwa chombo cha
utangazaji cha umma chenye wajibu wa kuhudumia watu wote.
Mkataba huo utahakikisha kuwa Shirika la Utangazaji Tanzania linatekeleza
malengo yake na kutumia mamlaka yake, linakuwa na uhuru wa kujieleza,
uhandishi wenye ubunifu na vipindi bila kuingiliwa na serikali na wadau wengine.
Washiriki walikuwa na maoni kwamba kiutendaji, TBC haikuwa na uhuru
wa kiuhariri na kwa ujumla ilionekana kutumikia maslahi ya serikali iliyopo
madarakani. Vilevile TBC inaonekana kama msemaji wa chama tawala na
mara nyingi hudhihirisha hujuma zisizochujwa dhidi ya upinzani na sauti
zenye ukinzani. Mmoja wa washiriki alisema kwamba watendaji na waandishi
wa habari halikadhalika wanalazimika ‘kuufyata’ mara wanapoajiriwa TBC na
kutekeleza sera za serikali, hata kama walikuwa wanahabari makini kabla ya
kuteuliwa kushika nafasi walizo nazo.
Washiriki walisema kwamba watendaji waliopita ambao walijaribu kuigeuza
TBC ili kuendana na uhuru wa uhariri na kuruhusu mawazo mchanganyiko
wamejikuta kwenye matatizo.

Alama:
Alama za mshiriki mmoja mmoja:
1

Nchi inakidhi kiashiria

2

Nchi inakidhi vipengele vichache tu vya kiashiria

3

Nchi inakidhi vipengele kadhaa vya kiashiria

4

Nchi inakidhi vipengele vingi vya kiashiria

5

Nchi inakidhi vipengele vyote vya kiashiria

Wastani wa alama:
Alama ya miaka iliyopita:

✓✓✓✓

✓

✓✓✓

✓

✓
✓

✓

1.4
2006: n/a; 2008: n/a; 2010: n/a; 2012: n/a; 2015: 2.2

3.6 Chombo cha umma kinapewa fedha za kutosha
kiasi cha kukilinda dhidi ya ushawishi wa kisiasa
kupitia bajeti yake na dhidi ya ulazima wa kufanya
biashara
Kulingana na washiriki, TBC haikuwa inapewa fedha za kutosha na gawio la
bajeti yake kwa mwaka kutoka wizarani linakidhi tu kulipa mishahara na mahitaji
ya msingi ya uendeshaji- na hii inaathiri maendeleo kibiashara na mpangilio wa
vipindi. Ili kuwafikia watu wengi, shirika limelazimika kuingia mkataba na redio

44

KIPIMO CHA VYOMBO VYA HABARI BARANI AFRIKA TANZANIA 2019

Select target paragraph3