ENEO LA 3

3.4 Vyombo vya serikali/umma vinawajibika kwa
umma kupitia bodi huru ambayo ina uwakilishi wa
jamii kwa ujumla na ambayo imeteuliwa kwa njia
iliyo huru na wazi.
TBC ilianzishwa mwaka 2007 chini ya Sheria ya Mashirika ya Umma ya
mwaka 2018. Inaongozwa na Mkurugenzi Mkuu na kusimamiwa na bodi ya
wakurugenzi. Mkurugenzi mkuu pamoja na mwenyekiti wa bodi wanateuliwa
na Rais, wakati wajumbe wengine wa bodi wanateuliwa na waziri, kila baada
ya kipindi cha miaka mitatu. Wajumbe wa bodi hawana uhakika wa kumaliza
kipindi chao kwa kuwa mamlaka ya uteuzi inaweza kutengua uteuzi wao kabla
ya kumaliza muda wao.
Washiriki walikuwa na maoni kwamba kwa kuangalia utaratibu wa uteuzi,
bodi ya TBC isingeweza kudhaniwa kuwa huru. Bodi iliyopo iliteuliwa mwaka
2016.23 Pamoja na tathmini hasi ya uhuru wake, washiriki hawawafahamu
wengi wa wajumbe wa bodi ya sasa na kwa hivyo wasingeweza kusema kama
waliwakilisha jamii kwa ujumla.

Alama:
Alama za mshiriki mmoja mmoja:
1

Nchi inakidhi kiashiria

2

Nchi inakidhi vipengele vichache tu vya kiashiria

3

Nchi inakidhi vipengele kadhaa vya kiashiria

4

Nchi inakidhi vipengele vingi vya kiashiria

5

Nchi inakidhi vipengele vyote vya kiashiria

Wastani wa alama:
Alama ya miaka iliyopita:

✓

✓

✓

✓

✓

✓✓✓
✓

✓✓

✓

1.6
2006: 1.5; 2008: 1.7; 2010: 1.9; 2012: 2.3; 2015: 2.1

3.5 Uhuru wa uhariri wa chombo cha umma/serikali
dhidi ya ushawishi wa kisiasa unalindwa na
sheria na unatumika kuhakikisha kwamba habari
zinakuwa za haki na zenye uwiano na zenye
kuakisi masuala yaliyopo
Sheria iliyounda TBC inaeleza kwamba ‘itahimiza mtizamo wa kitanzania kwa
kuwa na wigo mpana wa vipindi’. Katika Sehemu ya 7 (1-2), sheria ya TBC
23 Angalia taarifa mpya kupitia https://www.thecitizen.co.tz/News/Magufuli-appoints-new-TBC-board-chairman/18403403086330-rtfhwg/index.html.

43

KIPIMO CHA VYOMBO VYA HABARI BARANI AFRIKA TANZANIA 2019

Select target paragraph3