ENEO LA 2

Alama:
Alama za mshiriki mmoja mmoja:
1

Nchi inakidhi kiashiria

2

Nchi inakidhi vipengele vichache tu vya kiashiria

3

Nchi inakidhi vipengele kadhaa vya kiashiria

4

Nchi inakidhi vipengele vingi vya kiashiria

5

Nchi inakidhi vipengele vyote vya kiashiria

Wastani wa alama:
Alama ya miaka iliyopita:

✓✓

✓✓

✓

✓
✓✓

✓✓

✓

✓

3.2
2006: n/a; 2008: n/a; 2010: n/a ; 2012: n/a; 2015: 3.1

2.11 Nchi ina sera murua na kamilifu ya TEHAMA na/
au serikali inakuza na kutekeleza hatua ambazo
zinakidhi mahitaji ya mawasiliano kwa umma,
ikiwemo jamii za pembezoni
Tanzania ni kinara katika kubuni na kutumia Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
(TEHAMA) katika ukanda wa Afrika ya Mashariki. Washiriki walisema kwamba
Tanzania ni miongoni mwa nchi za mwanzo duniani kuunda teknolojia ya pochi
jongefu na ina utaalam wa hali ya juu wa tiba ya masafa. Kwa kutumia mpango
wa upatikanaji wa habari kwa wote, serikali hugharamia miradi ya kuunganisha
maabara za kompyuta mashuleni na mafunzo kwa vijana. Washiriki walieleza
kwamba serikali ilikuwa ikibuni njia za kusaidia mfumo wa teknolojia na
wajasiriamali chipukizi kwenye teknolojia kwa kutoa fedha na mfumo mahsusi
wa kodi kwa ajili ya kuwezesha mpango huo. Ushiriki wa serikali kwenye
TEHAMA umeleta matokeo chanya kwenye sekta mbalimbali; hasa benki,
biashara ya rejereja na biashara mtandao.
Sera mpya ya TEHAMA ilichapishwa mwaka 2016 kwa lengo la ‘kubadlisha
Tanzania kuwa na uchumi unaowezeshwa na TEHAMA, na ujuzi kupitia
ubunifu na matumizi endelevu ya TEHAMA ili kumnufaisha kila mwananchi na
biashara’.21 Washiriki walisema sera hiyo ilikuwa ya kimapinduzi na ilionesha
utashi wa kisiasa wa kujenga jamii yenye ujuzi.

21 Sheria ya Taifa ya TEHAMA, 2016.

37

KIPIMO CHA VYOMBO VYA HABARI BARANI AFRIKA TANZANIA 2019

Select target paragraph3