ENEO LA 2

michache tu iliyochunguzwa kila mwaka. Pamoja na hivyo, taarifa za habari kwa
ujumla zimejikita maeneo ya mijini. Ni kampuni chache tu zenye waandishi wa
habari kwenye maeneo ya pembezoni mwa nchi. Washiriki walieleza kwamba
jamii za vijijini zinapewa nafasi wakati wa ziara za viongozi wakuu wa serikali
kama vile ziara za mawaziri.

Alama:
Alama za mshiriki mmoja mmoja:
1

Nchi inakidhi kiashiria

2

Nchi inakidhi vipengele vichache tu vya kiashiria

3

Nchi inakidhi vipengele kadhaa vya kiashiria

4

Nchi inakidhi vipengele vingi vya kiashiria

5

Nchi inakidhi vipengele vyote vya kiashiria

Wastani wa alama:
Alama ya miaka iliyopita:

✓

✓

✓

✓✓

✓✓

✓

✓✓

✓

✓

2.6
2006: 3.1; 2008: 2.3; 2010: 3.2; 2012: 3.3; 2015: 3.9

2.10 Watangazaji binafsi wanatoa vipindi vyenye
viwango vinavyotakiwa vya maslahi ya umma
Watangazaji binafsi wanatakiwa na sheria ‘kukuza uwelewa wa wananchi
kuhusu masuala mbalimbali yenye maslahi ya kitaifa’ na ‘kutangaza na kuandika
habari au masuala yenye umuhimu kitaifa kama itakavyoelekezwa na serikali.’19
Washiriki walisema watangazaji binafsi wanajitahidi kuzingatia matakwa haya
lakini pia wanabanwa na hitaji la kuwafikia watu wengi ili kutengeneza vipindi
vyenye maslahi kwa umma. Hata hivyo, inaonekana kuwepo na kutoelewana
kati ya watangazaji na serikali kuhusu maana ya maslahi ya umma. Mathalan,
washiriki walieleza kwamba watangazaji walitozwa faini kwa kutoa taarifa
kuhusu madai ya kuwepo dosari wakati wa uchaguzi mdogo wa madiwani
tarehe 26 Novemba 2017.20

19 Sheria ya Vyombo vya Habari Tanzania, Kifungu cha 7.2.
20 Mamala ya Mawasiliano Tanzania yalivitoza faini vituo vitano vya luninga jumla ya TZS 60 milioni ($27,000) kwa utangazaji
‘usiozingatia sheria na maadili”. Vituo hivyo vilirusha hewani tathmini iliyofanywa na Kituo cha Sheria na Haki za
Binadamu (LHRC) kuhusu uchaguzi mdogo wa madiwani tarehe 26 Novemba, 2017, ambapo serikali iliona haukuzingatia
sheria wala maadili. Ilipatikana kwa anuani hii: https://www.africanews.com/2018/01/03/tanzania-fines-tv-stations-forairing-human-rights-report//

36

KIPIMO CHA VYOMBO VYA HABARI BARANI AFRIKA TANZANIA 2019

Select target paragraph3