ENEO LA 2

2.8 Vyombo vyote vya habari vinawakilisha
mchanganyiko wa wanajamii kwa haki
Tanzania ni jamii mchanganyiko ambayo ina makabila na lugha za kijamii zaidi
ya 120. Hata hivyo, mchanganyiko huu hauakisiwi kwenye vyombo vya habari
kwa kuwa sheria inazuia matangazo kwa lugha za kijamii. Kuruhusu matangazo
kwa ‘Kiingereza fasaha na Kiswahili pekee’ ni sehemu ya mkakati wa serikali
wa kudumisha umoja wa kitaifa na kuzuia uwezekanao wa makabila machache
kuwa na nguvu kuliko mengine. Hata hivyo, washiriki walikosoa njia hiyo kama
isiyo na ushahidi. ‘Hii inamkosesha mtanzania wa kawaida sauti kwenye vyombo
vya habari.’ ‘Sisi ni nchi yenye mchanganyiko lakini bado tuko mbali katika
kuukubali mchanganyiko na wingi wetu.’ Washiriki walisema pamoja na lugha,
kulikuwa na matatizo kuhusu namna ambavyo makundi mbalimbali ya kijamii
(hasa wale wachache) yanawakilishwa kwenye vyombo vya habari: kwa ujumla
vyombo vya habari hutengeneza imani potofu kuhusu Waarabu na Wahindi
wa Tanzania. Aidha, ni vipindi vichache sana huwalenga watu wenye ulemavu.
Matumizi ya lugha ya alama kwenye luninga ni nadra na hakuna magazeti
yanayotumia nukta nundu.

Alama:
Alama za mshiriki mmoja mmoja:
1

Nchi inakidhi kiashiria

2

Nchi inakidhi vipengele vichache tu vya kiashiria

3

Nchi inakidhi vipengele kadhaa vya kiashiria

4

Nchi inakidhi vipengele vingi vya kiashiria

5

Nchi inakidhi vipengele vyote vya kiashiria

Wastani wa alama:
Alama ya miaka iliyopita:

✓
✓

✓

✓

✓✓✓

✓✓

✓✓✓

2.2
2006: n/a; 2008: n/a; 2010: 2.6 ; 2012: 2.8; 2015: 3

2.9 Vyombo vya habari vinagusa maeneo yote ya
kiuchumi, kiutamaduni, kisiasa, mitazamo ya
kitaifa na kimaeneo, ikiwa ni pamoja na kwa njia
ya taarifa za kiuchunguzi
Tanzania itafanya uchaguzi mkuu mwaka 2020. Wakati wa AMB hii (takriban
mwaka mmoja kabla ya upigaji kura) washiriki walisema kwamba kulikuwa na
habari chache sana kuhusu uchaguzi huo. Walieleza kwamba ufinyu wa habari
kuhusu uchaguzi unaokaribia unaonesha kupungua kwa kasi kwa habari za
kisiasa kwa ujumla. Kutokana na athari za kuogofya za fursa za kisiasa zinazozidi
kudorora, waandishi wa habari wamegeukia kwenye mada ambazo zinadhaniwa
kuwa na hisia kidogo kama vile maslahi ya kibinadamu, utamaduni na shughuli
za serikali. Uhandishi wa habari za kiuchunguzi pia umeathirika, na ni miradi

35

KIPIMO CHA VYOMBO VYA HABARI BARANI AFRIKA TANZANIA 2019

Select target paragraph3