ENEO LA 2

2.3 Uhuru wa wahariri wa magazeti na vyanzo vya
habari mitandaoni zinazochapishwa na mamlaka
za umma unalindwa vya kutosha dhidi ya
kuingiliwa kisiasa kusiko kwa lazima
Tanzania ina magazeti mawili yanayomilikiwa na serikali, ambayo ni Daily News
na Habari Leo. Magazeti haya mawili na matoleo yake ya matandaoni kwa kiasi
kikubwa yanaonekana kama kipaza sauti cha serikali iliyoko madarakani na
sehemu ya nyenzo ya dola. Matokeo yake ni kwamba havina uhuru wa uhariri.
Washiriki waliezea utamaduni wa kuegemea upande mmoja, uchujaji habari/
kujichuja na uhandishi wa ‘mapambazuko’ kwenye magazeti yanayomilikiwa na
serikali. Pamoja na mambo mengine, wahariri na waandishi wa habari wa Daily
News na Habari Leo wana utaratibu wa kuzima habari ambazo siyo rafiki kwa
serikali na kunyamazisha sauti za watu wenye mawazo kinzani. Uchambuzi wa
maudhui kwenye gazeti la Daily News mwaka 2018 ulionesha kwamba gazeti
hilo halikuandika habari yoyote ya kuikosoa serikali kwa mwaka mzima. Mmoja
wa wanajopo alisema kwamba, ‘Unapokubali ajira Daily News, unajua moja kwa
moja kwamba kuna habari ambazo huwezi kugusa.’
Ingawa washiriki walikubaliana kwamba magazeti yanayomilikiwa na serikali
hayana uhuru wa uhariri, baadhi yao walidhani kwamba kukosekana kwa uhuru
kunaweza kusiwe na tatizo. Mmoja wa washiriki alisema kwa hisia kwamba
kama sehemu ya chombo cha serikali, magazeti yanayomilikiwa na serikali
yanapaswa kuangaliwa kama vyombo vilivyoko kwenye mikono ya mamlaka ili
kuchagiza utendaji wa serikali.

Alama:
Alama za mshiriki mmoja mmoja:
1

Nchi inakidhi kiashiria

2

Nchi inakidhi vipengele vichache tu vya kiashiria

3

Nchi inakidhi vipengele kadhaa vya kiashiria

4

Nchi inakidhi vipengele vingi vya kiashiria

5

Nchi inakidhi vipengele vyote vya kiashiria

Wastani wa alama:
Alama ya miaka iliyopita:

✓✓

✓✓

✓

✓
✓✓

✓

✓✓
✓

1.9
2006: 2.4; 2008: 1.8; 2010: 1.9; 2012: 2.3; 2015: 1.8

2.4 Uwazi wa umiliki wa vyombo vya habari
unatolewa na kulindwa na sheria
Umiliki wa vyombo vya habari Tanzania unathibitika kiraisi kwa vile mamlaka yana
orodha ya wamiliki wa makampuni na wadau chini ya Sheria ya Makampuni. Hata
hivyo, washiriki walisema kwamba daftari la umiliki wa makampuni linaweza
lisioneshe wamiliki halisi wa vyombo vya habari. ‘Watu wanaweza kuunda

31

KIPIMO CHA VYOMBO VYA HABARI BARANI AFRIKA TANZANIA 2019

Select target paragraph3