ENEO LA 1

1.9 Serikali haioneshi nia ya kuzuia au kuchuja habari
za mtandaoni isipokuwa kwa matakwa ya kisheria
ambayo yanaruhusu makatazo yanayohusiana
na maslahi halali na ambayo ni yalazima katika
jamii ya kidemokrasia na ambayo yanatumika na
mahakama huru
Washiriki walieleza kwamba kwa sababu ya sifa mbaya ya mamlaka kwa kujaribu
kuzuia uhuru wa habari, kulikuwa na uwezekano mkubwa kwamba serikali
ingechukua hatua madhubuti ili kuzuia au kuchuja habari mtandaoni. Pamoja
na kukosekana kwa ushahidi thabiti, maoni haya yanaonekana kuwa yamejikita
zaidi kwenye uelewa wa wananchi kwa sababu ya sera ya serikali. Mathalan,
hatua ya serikali ya kuunganisha Moduli ya Utambulisho wa Mtumiaji (SIM) wa
simu za mkononi na taarifa binafsi za mmiliki wa simu ya mkononi umesababisha
wasiwasi kwamba serikali ilikuwa na nia ya kufanya udukuzi mkubwa wa taarifa
za raia. Mmoja wa washiriki alidai kwamba kwa msaada wa China, kikosi cha
taifa cha makosa ya mtandaoni kilikuwa kimepata maarifa na uwezo mkubwa wa
kuingilia tovuti na kuzuia kusambaa kwa habari lengwa katika mtandao. Kipindi
cha uchaguzi mkuu wa mwaka 2015, mawasiliano kupitia Jamii Forums, jukwaa
la mjadala mtandaoni na jukwaa la kupuliza filimbi, ilizuiliwa kwa njia ya ajabu
kwa saa 24, na kusababisha wananchi kudhani kwamba mtandao huo ulikuwa
umetekwa na wataalam kutoka Ukraine au Urusi kwa niaba ya mamlaka. Pamoja
na ishara hizo za wazi za kuingilia habari mitandaoni, uhusika wa moja kwa moja
wa mamlaka unaonekana wa kudhaniwa zaidi kuliko wa kuthibitika.

Alama:
Alama za mshiriki mmoja mmoja:
1

Nchi inakidhi kiashiria

2

Nchi inakidhi vipengele vichache tu vya kiashiria

3

Nchi inakidhi vipengele kadhaa vya kiashiria

4

Nchi inakidhi vipengele vingi vya kiashiria

5

Nchi inakidhi vipengele vyote vya kiashiria

Wastani wa alama:
Alama ya miaka iliyopita:

25

✓

✓✓✓

✓

✓✓✓

✓

✓

✓
2.2
2006: n/a; 2008: n/a; 2010: 3.3; 2012: 4.5; 2015: 3.3

KIPIMO CHA VYOMBO VYA HABARI BARANI AFRIKA TANZANIA 2019

✓

Select target paragraph3