ENEO LA 1

Kuna sababu nyingi zinazofanya kuwe na mtizamo hasi. Kubwa kuliko zote
inaonekana kuwa kutokujitambua miongoni mwa wamiliki wa habari, kama
vile manispaa, Wakurugenzi Watendaji wa Wilaya (DEDs) na maafisa habari
kuhusu majukumu yao. Mmoja wa washiriki alielezea hali hii kama ifuatavyo,
‘Wakati mwingine, afisa habari anaweza akakuambia yeye si mzungumzaji
wa Mkurugenzi Mtendaji. Pamoja na kwamba sheria inampa mamlaka afisa
habari kutoa habari na kuwasaidia wale wanaotafuta habari, baadhi yao bado
watakuambia kwamba wanahitaji idhini ya wakuu wao wa kazi au DED. ‘Wakati
huo huo, baadhi ya wilaya zimeacha utaratibu wa kutoa taarifa kwa umma kwa
kutumia njia nyingine zilizokuwa zinatumia hapo kabla, kwa sababu wanahisi
kwamba taarifa zote kwa sasa lazima zitolewe na maafisa habari.’
Kwa kiasi kikubwa, washiriki waliona kwamba Sheria ya Upatikanaji wa Habari
ilikuwa imeirudisha nchi nyuma badala ya kuisaidia kusonga mbele. Walibainisha
kwamba umma haukuwa tena na uwezo wa kupokea taarifa kwa muda muafaka
kama ilivyokuwa hapo kabla wakati wilaya zilipokuwa na utaratibu wa kutumia
viongozi wa mtaa ili kuwasilisha taarifa kwa wapiga kura. Kwa kuzingatia wajibu
finyu wa kisheria wa kuheshimu maombi ya taarifa, mamlaka za umma zinatoa
tu taarifa ambazo zinakidhi maslahi yao, ambapo maslahi haya yanakuwa
hayana wigo mpana. Hata hivyo, kwa sababu za mahitaji ambatizi, baadhi ya
taasisi za umma kama vile Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) na Mamlaka ya
Mawasiliano (TCRA) mara nyingi hutoa taarifa kwa umma kwa wakati.

Alama:
Alama za mshiriki mmoja mmoja:
1

Nchi inakidhi kiashiria

2

Nchi inakidhi vipengele vichache tu vya kiashiria

3

Nchi inakidhi vipengele kadhaa vya kiashiria

4

Nchi inakidhi vipengele vingi vya kiashiria

5

Nchi inakidhi vipengele vyote vya kiashiria

Wastani wa alama:
Alama ya miaka iliyopita:

23

✓✓

✓

✓

✓✓

✓

✓

✓

✓

✓

2.2
2006: 1.1; 2008: 1.3; 2010: 1.6; 2012: 2.5; 2015: 1.6

KIPIMO CHA VYOMBO VYA HABARI BARANI AFRIKA TANZANIA 2019

✓

Select target paragraph3