ENEO LA 1

1.6 Vyanzo vya siri vya habari vinalindwa na sheria
na/au mahakama
Tanzania haina sheria mahsusi inayotoa ulinzi kwa vyombo vya habari. Sheria
kandamizi kama vile [Sheria ya Mpiga Filimbi na Shaidi] hazitumiki moja kwa
moja kulinda vyanzo vya siri vya habari. Hata hivyo, washiriki walisema kwamba
wananchi kwa ujumla wanajua kwamba waandishi wa habari hawatakiwi
kuweka bayana vyanzo vya siri vya habari kama kitu cha kawaida katika uhandishi
wa habari. Kwa hivyo, kwa kuzingatia kanuni hizi zinazokubalika kwa ujumla,
waandishi wa habari na taasisi za habari mara nyingi huwa wanaamua kulinda
vyanzo vyao vya habari.
Pamoja na hayo, kukosekana kwa kinga ya kisheria mara nyingi husababisha
bugudha kwa waandishi wa habari. Washiriki walisema kwamba ilikuwa
kawaida kwa waandishi wa habari kuteswa na kubinywa kwa njia nyinginezo
ili wabainishe vyanzo vyao vya habari. Mathalan, waendeshaji wa Jamii Forums,
jukwaa la mtandaoni ambalo huwawezesha wananchi ‘kuthubutu kuongea kwa
uhuru’, mara nyingi limekuwa kwenye mbinyo ili kubainisha utambulisho wa
wachangiaji wanaotumia majina bandia. Kwa mtazamo wa washiriki na taarifa
za habari, mwaka 2016 askari polisi waliwakamata waendeshaji wa jukwaa
hilo, Maxence Melo Mubyazi na Micke Williams na kuwafungulia mashtaka
kwa kuzuia haki kutendeka kwa kukataa kutoa taarifa za wanachama wao.14
Wawili hao walishtakiwa chini ya Sheria ya Makosa ya Kimtandao na endapo
watatiwa hatiani, watakabiliwa na adhabu ya kulipa hadi Shilingi milioni tatu za
Kitanzania; sawa na Dola 1,300 za Kimarekani, kifungo cha muda usiopingua
mwaka mmoja jela, au adhabu zote mbili. Waanzilishi hao wa ‘Jamii Forums
wamekuwa wakienda na kurudi mahakamani kwa vile mamlaka zinalazimisha
kupewa taarifa kuhusu wanachama.’

Alama:
Alama za mshiriki mmoja mmoja:
1

Nchi inakidhi kiashiria

2

Nchi inakidhi vipengele vichache tu vya kiashiria

3

Nchi inakidhi vipengele kadhaa vya kiashiria

4

Nchi inakidhi vipengele vingi vya kiashiria

5

Nchi inakidhi vipengele vyote vya kiashiria

Wastani wa alama:
Alama ya miaka iliyopita:

✓✓

✓

✓✓✓✓

✓✓

✓✓✓

2.3
2006: 1.6; 2008: 2.3; 2010: 1.8; 2012: 1.3; 2015: 1.2

14 Angalia kwa mfano taarifa ya habari ya BBC ya tarehe 16 Disemba 2016. Inapatikana mtandaoni kwa anuani hii://www.
bbc.com/news/world-africa-38341151. Mara ya mwisho ilipatikana tarehe 22 Mei 2019.

21

KIPIMO CHA VYOMBO VYA HABARI BARANI AFRIKA TANZANIA 2019

Select target paragraph3