ENEO LA 1

za nchi ‘kidogo kidogo’. Washiriki walikuwa pia na mtazamo kwamba mamlaka
zilionekana zaidi kutoitambua kabisa mikataba ya kimataifa, ambayo pia
inashindwa kuiheshimu. Mathalan, Tanzania haijatimiza wajibu wake wa kutoa
taarifa ya mara kwa mara kuhusu hali ya uhuru wa waandishi wa habari na haki
za binadamu kwa Umoja wa Afrika na Mkataba wa Umoja wa Mataifa kuhusu
Haki za Watu wenye Ulemavu, ambayo inazitaka nchi wanachama kutoa taarifa
kuhusu mambo hayo. Kwa kumalizia, mmoja wa washiriki alisema, ‘dhamira
yetu kwa viwango vya kimataifa vya haki za binadamu, hata kwenye mahakama,
ni ndogo sana kiasi kwamba hata huwa hatuna tabia ya kusema hilo.’
Kumekuwepo na jitihada za kupima hali ya pande mbili za Tanzania na tabia yake
ya kutoitambua mikataba ya kimataifa kwa ujumla wake. Mnamo mwaka 2019,
Mahakama ya Afrika Mashariki(EACJ) ilitoa uamuzi kwamba vipengele vingi
vya Sheria ya Vyombo vya Habari vilikuwa kinyume na uhuru wa kujieleza na
uhuru wa wanahabari kama ilivyoelezwa kwenye Mkataba ulioanzisha Jumuiya
ya Afrika Mashariki. Mahakama ya Afrika ya Mashariki iliitaka Tanzania kufuta
vipengele hivyo, hasa vile vinavyohusu uchochezi, udhalilishaji na utoaji wa
taarifa za uongo. Umoja wa Uhuru wa Vyombo vya Habari uliipongeza hukumu
hiyo11 kama hatua muhimu katika kupigania uhuru wa kujieleza na uhuru wa
vyombo vya habari Tanzania ambao unaendelea kuzorota. Tanzania imekata
rufaa dhidi ya hukumu hiyo na wakati AMB ikiendelea, vipengele kandamizi vya
Sheria ya Vyombo vya Habari vilikuwa bado vinatumika.

Alama:
Alama za mshiriki mmoja mmoja:
1

Nchi inakidhi kiashiria

2

Nchi inakidhi vipengele vichache tu vya kiashiria

3

Nchi inakidhi vipengele kadhaa vya kiashiria

4

Nchi inakidhi vipengele vingi vya kiashiria

5

Nchi inakidhi vipengele vyote vya kiashiria

Wastani wa alama:
Alama ya miaka iliyopita:

✓

✓

✓✓✓✓✓✓

✓

✓✓

✓

2 .1
2006: n/a; 2008: n/a; 2010: 2.2; 2012: 3.3; 2015: 2.5

1.5 Machapisho hayahitaji kupata kibali cha
kuchapisha kutoka kwa mamlaka husika
Nchini Tanzania, ni kinyume cha sheria kuchapisha gazeti na vyanzo vingine
vya habari kwa maandishi bila kupata kwanza leseni kutoka serikalini. Hitaji hili
la leseni linahusu kuuza, kusambaza, kuingiza na kutoa habari kwa maandishi
popote nchini. Sheria hii inampa mamlaka Mkurugenzi wa Idara ya Huduma za
Habari au mwakilishi wake kukataa maombi ambayo hayakidhi matakwa ya leseni
na pia kufungia au kufuta leseni ‘endapo mwenye leseni anashindwa kuzingatia
11 Angalia kwa mfano CPJ. Inapatikana mtandaoni kwa anuani: https://cpj.org/2019/03/east-african-court-rules-thattanzanias-media-serv.php.

19

KIPIMO CHA VYOMBO VYA HABARI BARANI AFRIKA TANZANIA 2019

Select target paragraph3