ENEO LA 1

uhuru wa vyombo vya habari. Washiriki walitoa mfano wa Sheria ya Magereza,
Sheria ya Makosa ya Kimtandao, Sheria ya Usalama wa Taifa, Sheria ya Maeneo
na Sehemu Zilizozuiliwa, Sheria ya Watu Wasiokubalika na hata Sheria ya
Huduma za Vyombo vya Habari kama miongoni mwa sheria kandamizi zaidi na
zenye kutumiwa mara nyingi.
Sheria ya Maeneo na Sehemu Zilizozuiliwa, kama ilivyo Sheria ya Watu
Wasiokubalika, iko nje kabisa ya mipaka ambayo inaweza kuwa na tafsiri anuai na
zinazoweza kukiukwa kwa urahisi. Sheria hii inazuia matumizi ya umma ya taarifa
zinazopatikana kwenye sehemu zilizoainishwa kwamba zimezuiliwa (kwa mtizamo
wa waziri mwenye dhamana), bila kujali kwamba ina maslahi halali ya umma
na ya kiusalama). Mmoja wa wanajopo alisema kwamba umma haukujulishwa
kuhusu orodha ya maeneo na sehemu ambazo zimezuiliwa, lakini bado wakiukaji
wanakabiliwa na hatari ya kifungo cha miaka 20 gerezani endapo watatiwa hatiani.
Washiriki walibainisha kwamba kwa kadri itakavyokuwa na mashiko ya
kisheria, serikali ina kawaida ya kufukua sheria zilizokwishakusahaulika zamani
na kuzitumia. ‘Hatuzungumzii tena sheria hizi kandamizi kwa vile hatutaki
kuwakumbusha uwepo wake.’

Alama:
Alama za mshiriki mmoja mmoja:
1

Nchi inakidhi kiashiria

2

Nchi inakidhi vipengele vichache tu vya kiashiria

3

Nchi inakidhi vipengele kadhaa vya kiashiria

4

Nchi inakidhi vipengele vingi vya kiashiria

5

Nchi inakidhi vipengele vyote vya kiashiria

Wastani wa alama:
Alama ya miaka iliyopita:

✓

✓

✓

✓

✓✓✓
✓

✓

✓
✓

✓

1.8
2006: n/a; 2008: n/a; 2010: n/a; 2012: n/a; 2015: 1.8

1.4 Serikali inaheshimu mikataba ya kikanda na ile ya
kimataifa kuhusu uhuru wa kujieleza na uhuru wa
vyombo vya habari
Tanzania ni nchi ya pande mbili – ni istilahi ya kitaalam inayotumiwa na sheria
ya kimataifa kuelezea nchi ambayo inazitenga sheria zake za ndani na mikataba
ya kimataifa na mikataba mingineyo. Matokeo yake, mikataba ya kimataifa
inayoridhiwa na Tanzania haichukuliwi kama sheria moja kwa moja. Endapo
mikataba hiyo haijapata ‘tafsiri’ ya sheria za kitaifa, haitambuliki kama sheria ndani
ya Tanzania. Wanajopo walisema kwamba kwa sababu ya utaratibu huu, mikataba
ya kimataifa inayohusu uhuru wa kujieleza ambao imeridhiwa na Tanzania ni
vigumu kuheshimiwa nchini.
Washiriki walieleza kwamba, pale serikali inapoona mikataba ya kimataifa inafaa
kwa maslahi yake, basi vifungu vya mikataba hiyo hujumuishwa kwenye sheria

18

KIPIMO CHA VYOMBO VYA HABARI BARANI AFRIKA TANZANIA 2019

Select target paragraph3