ENEO LA 1

yamekosolewa na watu na taasisi mbalimbali kwamba ni kinyume na sheria5
lakini bado yameendelea kutumika. Mwezi Machi 2019, pamoja na sababu
nyinginezo, sheria hii ilitumika kufungia kwa muda gazeti la The Citizen kwa
kuandika habari bila kibali kuhusu viwango vya ubadilishaji fedha za kitanzania
dhidi ya Dola ya Kimarekani.6 Mamlaka zilisema kwamba gazeti hilo lilifungiwa
kwa kurudia kutoa taarifa za uongo na za kichochezi. Hata hivyo, mmoja wa
wanajopo alisema, ‘Taarifa hizo zilikuwa za kweli. Tatizo ni kwamba uthibitisho
wa taarifa hizo haukufanywa na NBS’.
Kwa mujibu wa wanajopo, hujuma dhidi ya uhuru wa habari na uandishi wa
habari unaanzia kwenye matumizi mabaya ya sheria hadi mashambulizi ya ana
kwa ana ya kimwili. Kati ya mwaka 2016 na 2017, Kituo cha Sheria na Haki za
Binadamu (LHRC), ambacho ni taasisi isiyo ya kiserikali, kiliorodhesha matukio 17
ya unyanyasaji dhidi ya waandishi wa habari na watetezi wa haki za binadamu
na matukio mengine mengi dhidi ya raia wengine.7 Mwandishi wa habari za
kiuchunguzi Azory Gwanda alitoweka mwezi Novemba 2017, na hadi wakati
wa kuchapisha taarifa hii hakuna taarifa yoyote kama bado yuko hai. Asasi za
kiraia wanakosoa kutokufanyika kwa uchunguzi wa tukio hili. Kwa mujibu wa
wanajopo na Article 19 Eastern Africa, Gwanda alikuwa akichunguza matukio ya
mauaji yaliyolenga viongozi wa kimaeneo na maafisa usalama, baadhi ya matukio
hayo yakidaiwa kufanywa na ‘washambuliaji wapanda pikipiki wasiojulikana’,
wakati alipochukuliwa na watu wasiojulikana asubuhi ya tarehe 21 Novemba
2017.8
Utata unaoonekana wa serikali dhidi ya uhuru wa kujieleza umeibua woga.
Wanajopo walibainisha kwamba waandishi wa habari na taasisi za vyombo vya
habari wamelazimika kujichuja wenyewe na hivyo kuwa waangalifu na kuchagua
habari za kuandika kwa sababu hatari ya kuadhibiwa imekuwa kubwa. Mmoja
wa washiriki alielezea mazingira ya sasa kama ifuatavyo:
Waandishi wa habari watakuambia kwamba hawako huru. Sasa hivi,
kama unataka kupata mafanikio katika uandishi wa habari, ni lazima
uimbe nyimbo za kuitukuza serikali au uandike habari zile tu ambazo
wale walioko madarakani wanataka kuzisikia. Uandishi wa habari
za kiuchunguzi hazina mpango tena Tanzania. Hata kutoa taarifa za
matukio kwa sasa ni hatari sana. Kwa mfano, mamlaka ziliweka adhabu
ya shilingi milioni 60 (Dola za Kimarekani 27,000) kwa vituo vya luninga

5

6

7

8

Angalia: Benki ya Dunia (2018). Taarifa ya Benki ya Dunia kuhusu Marekebisho ya Sheria ya Takwimu ya Tanzania ya
mwaka 2015. Inapatikana mtandaoni kwa anuani hii: https://www.worldbank.org/en/news/statement/2018/10/02/worldbank-statement-on-amendments-to-tanzanias-2015-statistics-act. Mara ya mwisho ilipatikana tarehe 20 Mei 2019.
Angalia gazeti la Daily Monitor (linapatikana mtandaoni kwa anuaani hii: https://www.monitor.co.ug/News/National/
Tanzania-bans-Citizen-newspaper/688334-5002850-r04jl4z/index.html) na CPJ (Inapatikana mtandaoni kwa anuani hii:
https://cpj.org/2019/03/tanzania-citizen-7-day-publication-ban.php) Taarifa zote mbili zilipatikana tarehe 20 Mei 2019.
FIDH and LHRC (2017). Tanzania: Uhuru wa Kujieleza Mashakani, Joint Situation Note. No 698a. Inapatikana mtandaoni
kwa anuani hii:: https://www.fidh.org/IMG/pdf/joint_position_note_tanzania_fidh_lhrc.pdf. Mara ya mwisho ilipatikana
tarehe 21 Mei 2019.
Angalia Article 19 East Africa. Linapatikana mtandaoni kwa anuani: https://www.article19.org/resources/tanzaniaconcern-grows-missing-journalist-azory-gwanda/. Mara ya mwisho kupatikana ilikuwa tarehe 20 Mei 2019.

15

KIPIMO CHA VYOMBO VYA HABARI BARANI AFRIKA TANZANIA 2019

Select target paragraph3