ENEO LA 1

ambayo ingekuwa na mabadiliko chanya, ambayo inatoa uhuru kwa vyombo
vya habari, imefungiwa ndani na hivyo kufifisha matumaini kuleta mabadiliko
kwenye hali ya vyombo vya habari wakati wowote kwa siku za karibuni.

Alama:
Alama za mshiriki mmoja mmoja:
1

Nchi inakidhi kiashiria

2

Nchi inakidhi vipengele vichache tu vya kiashiria

3

Nchi inakidhi vipengele kadhaa vya kiashiria

4

Nchi inakidhi vipengele vingi vya kiashiria

5

Nchi inakidhi vipengele vyote vya kiashiria

Wastani wa alama:
Alama ya miaka iliyopita:

✓

✓✓

✓

✓✓✓✓✓✓✓

✓

2.3
2006: 2.8; 2008: 2.4; 2010: 2.7; 2012: 2.5; 2015: 2.7

1.2 Haki ya uhuru wa kujieleza inatumiwa na
wananchi, wakiwemo waandishi wa habari, bila
hofu
Mwaka 2017, Tanzania iliyafungia magazeti manne kwa muda, na hiki kilikuwa
kitendo cha aina yake kufanyika ndani ya mwaka mmoja katika historia ya hivi
karibuni ya Tanzania. Hatua hii iliongeza idadi ya machapisho yaliyofungiwa kufikia
matano katika kipindi cha miaka miwili na ilidhihirisha mwendelezo wa mazingira
mabaya na yenye changamoto kwa tasnia ya uhandishi wa habari na uendeshaji
wa vyombo vya habari. Hatua hiyo ilifuatiwa na maonyo na kukumbushia
kulikofanywa na Rais kwamba upashaji habari Tanzania unapaswa kuzingatia
maadili. Mwezi Oktoba mwaka 2017, Bwana Henry Maina, Mkurugenzi wa
Kanda wa Article 19 Eastern Africa, shirika lisilo la kiserikali lenye kujishughulisha
na haki za vyombo vya habari, alisema kwamba, ‘Kufungiwa kwa magazeti ni
hujuma dhidi ya uhuru wa vyombo vya habari nchini na kunadhoofisha wajibu wa
vyombo vya habari kama waangalizi katika jamii ya kidemokrasia. Ni habari mbaya
kwamba Tanzania inaonekana kurudi nyuma katika dhamira yake ya kutoa uhuru
kwa vyombo vya habari kwa kufungia taasisi za habari bila sababu za msingi.
Kufungia vyombo vya habari kama hivi kunaweza pia kusababisha waandishi wa
habari kujihariri wenyewe na hivyo kuchagua habari.’4
Wanajopo walisema kwamba serikali imetumia sheria kandamizi na mamlaka
yake makubwa kukanyaga uhuru wa kujieleza. Moja kati ya silaha ya hatari
kabisa zilizo kwenye mikono ya mamlaka ni sheria mpya ambayo inazuia
matumizi ya takwimu rasmi bila idhini. Marekebisho ya mwaka 2018 ya Sheria
ya Taifa ya Takwimu ya mwaka 2015 inataka idhini ya Ofisi ya Taifa ya Takwimu
(NBS) kabla ya kuchapisha takwimu rasmi; serikali ilidai kwamba marekebisho
haya yalihitajika ili kulinda ukweli na uhalisi wa takwimu. Marekebisho haya
4

14

https://www.article19.org/resources/tanzania-ban-on-newspapers-raises-concerns-for-press-freedom/.

KIPIMO CHA VYOMBO VYA HABARI BARANI AFRIKA TANZANIA 2019

Select target paragraph3