ENEO LA 1

mahakama yoyote ya masuala ya madai au ya jinai; kulinda heshima,
haki na uhuru wa watu wengine au usiri wa watu wanaohusika katika
mashauri mahakamani, kuzuia utoaji wa taarifa za siri, au kulinda
heshima, mamlaka na uhuru wa mahakama; kuzuia uundwaji, usimamizi
na shughuli za taasisi na mashirika binafsi nchini; au kitu kingine
chochote kitakachofanyika kwa ajili ya kuendeleza au kuhifadhi maslahi
ya taifa kwa ujumla.
Kinyume na kanuni inayokubalika kwa ujumla ambayo inachukulia katiba kama
sheria mama, wanajopo walisema kwamba inapofika suala la haki na uhuru,
Katiba ya Tanzania inapwaya. Walirudia na kunukuu Kifungu cha 30(5) cha Katiba
hiyo, ambapo walisema kwamba ni vigumu kudai haki na uhuru wa kikatiba
kwa kuwa inawapa majaji mamlaka kuvuka mipaka ya kikatiba panapokuwepo
mgongano wa kimaslahi. Kifungu hicho kinaeleza kwamba:
Katika shauri lolote, inapodaiwa kwamba sheria yoyote iliyotungwa au
hatua yoyote itakayochukuliwa na serikali au mamlaka nyingine yoyote
inavunja au kuminya haki yoyote ya msingi, uhuru na wajibu kama
ilivyoelezwa kwenye vifungu vya 12 hadi 29 vya Katiba hii, na Mahakama
Kuu ikajiridhisha kwamba sheria au kitendo husika, kwa kadri kwamba
inakinzana na Katiba hii, ni batili, au ni kinyume na Katiba hii, Mahakama
Kuu, kama ikiona hivyo, au kama mazingira au maslahi ya umma yanahitaji
hivyo, badala ya kuamua kwamba sheria hiyo au kitendo hicho ni batili,
itakuwa na mamlaka ya kuamua kuipa serikali au mamlaka nyingine
inayohusika muda wa kurekebisha kasoro zilizobainishwa kwenye sheria
au kitendo husika kwa muda na namna ambavyo Mahakama Kuu
itaamua, na sheria hiyo au kitendo hicho kitahesabika kuwa halali hadi
pale kasoro hizo zitakapokuwa zimerekebishwa au muda utakaowekwa
na Mahakama Kuu utakapokuwa umemalizika, kutegemeana na kipi
kinatangulia.
Pamoja na mianya iliyopo kwenye Katiba, wanajopo waliona kwamba vipengele
mbalimbali vya sheria vimepitishwa na mara nyingi vinasimamiwa ambavyo
vinakiuka vifungu vya Katiba ambavyo vinatoa uhuru wa kujieleza. Baadhi ya
sheria mbaya kabisa ni pamoja na Sheria ya Makosa ya Mtandaoni na Sheria
ya Magereza. Baadhi ya sheria hizi zimeibuka hivi karibuni kabisa na mifano
mizuri ni Sheria ya Vyombo vya Habari ya Mwaka 2016, ambayo kwa mara
nyingine imeingiza makosa ya uchochezi na kutoa kashfa, ikiwemo kuwakashfu
marehemu. Wanajopo walisema kwamba kiujumla, kuna dalili za kutungwa kwa
sheria kandamizi zaidi ambazo zinaweka vigingi kwa watu na taasisi kutumia
haki yao ya uhuru wa kujieleza na uhuru wa vyombo vya habari. Wakitolea
mfano Sheria ya Vyombo vya Habari, mmoja wa washiriki alisema, “Sheria ya
Magazeti ya Mwaka 1976, ambayo ilionekana kuwa kandamizi, ilirithiwa na
sheria kandamizi zaidi, yaani Sheria ya Vyombo vya Habari. Tuliomba mkate na
badala yake tukapewa nyoka.”
Kwa muhtasari, washiriki walionesha kwamba pamoja na kwamba Katiba
inatambua uhuru wa kujieleza kama haki, inashindwa kuilinda haki hizo,
haizungmzii uhuru wa vyombo vya habari na imeacha mianya inayoruhusu
kushamiri kwa sheria nyingine ambazo zinaweza kukiuka haki hizo. Katiba

13

KIPIMO CHA VYOMBO VYA HABARI BARANI AFRIKA TANZANIA 2019

Select target paragraph3