ENEO LA 1

(1) Kila mtu ana haki na uhuru wa (a) kutafuta, kupata, na kutoa habari
na taarifa; na (b) kuanzisha chombo cha habari na njia nyinginezo za
kusambaza habari bila kujali mipaka ya kitaifa.
(2) Vyombo vya habari vitakuwa huru na vitakuwa na (a) haki ya kupata,
kutumia na kutoa habari na taarifa wanazopata; (b) jukumu la (i) kutoa
habari na taarifa kwa umma; na (ii) kuheshimu na kulinda utu, heshima,
uhuru na hadhi ya raia dhidi ya habari na taarifa wanazopokea, kuandaa
na kusambaza.
(3) Serikali na taasisi zake, asasi za kiraia na watu binafsi watawajibika
kwa kutoa taarifa kwa umma kuhusu shughuli na utekelezaji wa
shughuli zao.
(4) Bunge litatunga sheria kwa minajili ya kulinda: (a) haki na uhuru
wa vyombo vya habari; na (b) habari na taarifa kwa minajili ya usalama
wa taifa, amani, maadili ya umma, haki, heshima na uhuru wa watu
wengine.
Pamoja na mtizamo wake chanya, wanajopo wamebaini kwamba uhuru wa
vyombo vya habari uliopendekezwa kwenye katiba mpya haukuwa na tija kama
katiba mpya itaendelea kufungiwa kwenye makabati- kama hali ilivyokuwa
wakati wa kufanya tathmini hii ya hali ya vyombo vya habari kwa Tanzania.
Aidha, wanajopo walikuwa na mtizamo usioridhisha kwa ujumla kuhusu kiasi
ambacho katiba iliyopo inatoa uhuru wa kujieleza na uhuru wa vyombo vya
habari:
Kueleza [uhuru wa kujieleza] kwenye katiba ni kitu kimoja, kutoa uhuru
huo ni kitu kingine. Kutoa ina maana kwamba hatua zinachukuliwa
kuhakikisha kwamba raia wanapata haki hizo. Lakini hali ni tofauti.
Kusema kweli, hakuna haki yoyote inayotolewa katika nchi ya Tanzania.
[Badala yake] sheria zinazotakiwa kuchagiza haki hizi zimetengenezwa
kwa mtindo wa kuzidhoofisha haki hizo.
Katiba yenyewe pia imeweka mipaka katika kutumia haki hizo na uhuru huo,
ikizingatiwa kwamba kifungu cha 30 kinaeleza kwamba haki zinatumiwa pale tu
zinapokuwa hazikiuki haki za watu wengine na maslahi mapana. Na kwa kukazia
zaidi, kifungu hicho kinaongezea kwamba vifungu vya katiba vinavyoainisha
haki za msingi za binadamu, uhuru na wajibu haviizuii serikali kusimamia sheria
zilizopo au kutunga sheria nyingine ambazo zinaweza kuathiri haki na uhuru wa
raia ulioainishwa kwenye katiba. Kwa mfano, katiba inabainisha kwamba haki,
uhuru na wajibu wa raia vinaweza kuingiliwa kwa madhumuni ya:
Kuhakikisha kwamba haki na uhuru wa watu wengine au maslahi ya
umma hayazuiliwi na matumizi mabaya ya uhuru na haki za watu binafsi;
Kuhakikisha kwamba ulinzi, usalama wa umma, utulivu wa umma,
maadili ya umma, afya ya jamii, mipango ya mijini na vijijini, uchimbaji
na matumizi ya madini au kuongeza na kuendeleza mali au maslahi
mengine yoyote kwa ajili ya kuimarisha maslahi ya umma; kuhakikisha
utoaji maamuzi au amri ya mahakama inayofanya au kutolewa katika

12

KIPIMO CHA VYOMBO VYA HABARI BARANI AFRIKA TANZANIA 2019

Select target paragraph3