Ingawa huduma za matangazo (hasa kwa njia ya redio) zinapatikana kwenye
sehemu kubwa ya nchi, kuna mawanda finyu sana kwenye vyombo vya habari.
Tanzania ni jamii mchanganyiko yenye makabila zaidi ya 120 pamoja na lugha
za kijamii, lakini mchanganyiko huu haujidhihirishi kwenye vyombo vya habari
kwa sababu sheria inazuia matumizi ya lugha za kijamii kwenye vyombo vya
habari. Shirika la utangazaji la taifa -Shirila la Utangazaji Tanzania (TBC), ambalo
linatakiwa kuwafikia watu wote, linadhibitiwa vikali na hutumiwa kama kipaza
sauti cha serikali au chama tawala, na hivyo kuzima sauti za watu wenye mawazo
mbadala.
Sauti za wanawake mara nyingi huzimwa kwenye vyombo vya habari. Kwa mujibu
wa mtandao wa GenderLinks, wanaume bado wanatawala kwenye vyombo
vya habari Tanzania.1 Wanawake wanaofanya kazi kwenye vyombo vya habari
pia hunyanyaswa kijinsia. Utafiti uliofanywa na Internews kuhusu mchango wa
wanawake kwenye vyombo vya habari ulionesha kukithiri kwa unyanyasaji wa
kijinsia kwenye taasisi zote za habari.2 Wanawake pia wanazungumziwa vibaya
na viongozi wa serikali na vyombo vya habari.
Mazingira ya vyombo vya habari na waandishi wa habari yamedorora kwa
kiasi kikubwa katika miaka ya karibuni; na kwa uchache, magazeti manne
yamefungiwa tangu mwaka 2017. Sheria kandamizi, matumizi ya adhabu kubwa
na kukamatwa bila kushtakiwa ni baadhi ya mambo yanayowakuta waandishi
wa habari. Vilevile, mwanahabari Azory Gwanda ametoweka nyumbani tangu
mwezi Novemba 2017. Kabla ya kutoweka, alikuwa ameandika makala kadhaa
yaliyoelezea mauaji ya viongozi wengi wa kimaeneo na maofisa wa polisi.
Kutoweka kwake kumesababisha hali ya sintofahamu kwa vyombo vya habari.
Waandishi wa habari na vyombo vya habari wamelazimishwa kujihariri wenyewe.
Hali ya sintofahamu haipo tu kwa vyombo vya habari lakini pia inawapata hata
wanajamii. Watu wanaogopa kubadilishana mawazo ya kisiasa kwa uhuru na
angalizo hili limeingia pia kwenye mijadala mitandaoni.
Changamoto nyingine kama vile kushuka kwa viwango vya utoaji taarifa, na
rushwa kwa ujumla wake pia zinavikabili vyombo vya habari. Kwa mfano, haki
na usahihi katika utoaji habari vinazidi kuporomoka kutokana na sababu anuai
kama vile mafunzo hafifu, uharakishaji unatokana na hitaji la kwenda na muda
na kuondoka kwa wanahabari nguli. Mbaya zaidi, waandishi wa habari wa
Tanzania hawalipwi vizuri. Waandishi wengi hawana mikataba ya ajira, na kwa
hivyo, hawapati mafao wanayostahili. Kwa kukosa umoja katika kushughulikia
kero zao, waandishi wengi hujihusisha na rushwa. Uhandishi wa habari wa
bahasha ya kahawia, ambapo waandishi wa habari hupewa bakhshishi ya fedha
ili kuandika habari kwa upendeleo au kuzima habari zenye taswira hasi, unazidi
kushika kasi nchini.
Pamoja na hali ya kusikitisha ya hali ya kisiasa na vyombo vya habari, bado kuna
matumaini. Ingawa taasisi za kiraia zimekuwa zikilalamikia kuongezeka kwa
1
2

8

Jambo hili liliibuliwa na Mkurugenzi Mtendaji wa GenderLinks, Colleen Lowe Morna, kwenye Mkutano wa Kilele kuhusu
Jinsia na Upashaji Habari kuhusu Maendeleo Endelevu uliofanyika Tanzania mwaka 2018.
Taarufa ya Uchambuzi wa Usawa wa Kijinsia na Ushirikishaji wa Kijamii uliofanywa na FHI 360 kwa ushirikiano na
Internews.

KIPIMO CHA VYOMBO VYA HABARI BARANI AFRIKA TANZANIA 2019

Select target paragraph3