mbinyo wa serikali mwaka mzima kwa njia ya vitisho, uchunguzi, ukamataji
na sheria kali, taasisi za kiraia Tanzania (CSOs) na mashirika yasiyo ya kiserikali
(NGOs) bado vina nguvu. Mara nyingi asasi za kiraia huungana na kuchagiza
mapambano dhidi ya sheria ambazo zinaathiri uhuru wa vyombo vya habari.
Muungano wa Haki ya Habari umeweza kuunganisha nguvu ya taasisi kadha wa
kadha za kiraia kuongoza mapambano ya kimkakati dhidi ya sheria kandamizi
za vyombo vya habari. Muungano wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania
na Jukwaa la Muungano wa Asasi za Kiraia Afrika Mashariki wanasifika pia kwa
kuchukua hatua dhidi ya masahibu ya vyombo vya habari. Mfano wa hivi karibuni
ni mapema mwaka 2019 ambapo mashirika matatu yasiyo ya kiserikali Tanzania
yalifungua mashtaka dhidi ya Sheria ya Vyombo vya Habari kwenye Mahakama
ya Afrika Mashariki (EACJ). Mahakama hiyo iliamua kwamba vipengele anuai vya
Sheria ya Vyombo vya Habari vinaminya uhuru wa vyombo vya habari na uhuru
wa kujieleza, na hivyo kuitaka serikali ya Tanzania kuifutilia mbali sheria hiyo.
Tanzania inaelekea kwenye uchaguzi mkuu mwaka 2020. Tangu ilipohama
kutoka kwenye nchi ya chama kimoja cha siasa na kwenda kwenye mfumo wa
vyama vingi, Tanzania imekuwa inafanya chaguzi za amani kwa kiasi fulani. Hata
hivyo, mgawanyiko wa kisiasa unaozidi kuongezeka hivi sasa unaashiria wasi
wasi mkubwa katika chaguzi hizi zinazokuja. Kama ilivyo kwa chaguzi nyinginezo
duniani, kuna ongezeko katika matumizi ya wataalam wapotoshaji kwenye
mitandao ya kijamii ili kupindisha mawazo na mitizamo huru. Upotoshaji huu
unaofanyika kwa njia ya mtandao pamoja na kujitafutia umaarufu wa kisiasa na
mabadiliko katika uthibiti unachangia sana kushusha kiwango cha chaguzi huru
na za haki ambazo zimeiletea Tanzania sifa kubwa katika ukanda wa Afrika ya
Mashariki.
Mjadala huu ulifanyika kwenye hoteli ya White Sands, Dar es Salaam,
Tanzania Mei 2019.

9

KIPIMO CHA VYOMBO VYA HABARI BARANI AFRIKA TANZANIA 2019

Select target paragraph3