Kwa miaka ya 2009, 2013 na 2019, baadhi ya viashiria vilibadilishwa ili kuakisi
mabadiliko katika hali ya vyombo vya habari. Matokeo yake ni kwamba, kwenye
baadhi ya maeneo, ulinganishi wa viashiria vya taarifa zilizopita hauendani kwa
vile kiashiria ama ni ingizo jipya au kimefanyiwa marekebisho makubwa.
Majumuisho ya kipengele kimojakimoja yanagawanywa kwa idadi ya wanajopo
ili kukokotoa wastani wa alama kwa kila kiashiria. Wastani wa alama katika kila
kiashiria unajumlishwa ili kupata wastani wa alama katika eneo lengwa.
Matokeo
Taarifa ya mwisho ya kitaamuli inatoa muhtasari wa maelezo ya jumla ya mjadala
ambao huonesha wastani wa alama kwa kila kiashiria. Majina ya wanajopo
hayatambulishwi kwenye taarifa ili kuwaepusha na madhara yanayoweza
kuwapata kutokana na michango yao katika mijadala. Taarifa hizi zinaweza
kutumiwa kama nyenzo ya kuibua mjadala wa kisiasa kuhusu marekebisho ya
mazingira ya vyombo vya habari.
Katika nchi ambazo Kiingereza siyo lugha rasmi, taarifa huchapishwa katika
lugha mbili.
Ili kuwafanya AMB, FES na MISA kubakia kama wenyeji wa wanajopo na watoaji
wa zana za utafiti, yaliyomo katika majadiliano pamoja na taarifa hubakia kuwa
mali ya jopo la wataalam wa ndani ya nchi na hayawakilishi au kuakisi maoni ya
FES au MISA.
Kufikia mwishoni mwa mwaka 2019, AMB ilikuwa imeshakamilika kwa
mafanikio mara 121 katika nchi 32 za kiafrika, na katika baadhi ya nchi hizo
ikiwa ni kwa mara ya sita tayari.
Luckson Chipare
Mkurugenzi wa Kanda
Taasissi ya Vyombo vya Habari
Afrika Kusini (MISA)
Windhoek, Namibia

3

Freya Gruenhagen
Mkurugenzi
fesmedia Africa
Friedrich-Ebert-Stiftung
Windhoek, Namibia

KIPIMO CHA VYOMBO VYA HABARI BARANI AFRIKA TANZANIA 2019

Select target paragraph3