Kipimo cha Vyombo vya Habari Barani
Afrika
Kipimo cha Vyombo vya Habari Barani Afrika (AMB) ni tathmini yakinifu na
kamilifu; na mfumo wa upimaji wa mazingira ya kitaifa ya vyombo vya habari
katika bara la Afrika. Tofauti na tafiti nyingine zinazohusu vyombo vya habari au
vipimo vya vyombo vya habari, AMB ni tathmini rejeshi yenye kuzingatia vigezo
vya ndani ya nchi vinavyotokana na Mikataba na Maazimio ya Afrika kama
vile Azimio la Kanuni za Uhuru wa Kujieleza Afrika la mwaka 2002 lililotolewa
na Tume ya Afrika ya Haki za Binadamu na Haki za Watu. Zana za utafiti huu
ziliundwa kwa ushirikiano kati ya fesmedia Africa, ambao ni mradi wa vyombo
vya habari wa Friedrich-Ebert-Stiftung (FES) barani Afrika, na Taasisi ya Vyombo
vya Habari Kusini mwa Afrika (MISA) mnamo mwaka 2004.
AMB ni uchambuzi unaolenga kupima hali ya vyombo vya habari katika nchi
husika na wakati huohuo kuwa kama nyenzo ya kushawishi uboreshaji wa
mazingira ya vyombo vya habari. Matokeo ya utafiti hutolewa kwa wananchi wa
nchi husika ili waweze kushawishi maboresho ya hali ya vyombo vya habari kwa
kuzingatia Maazimio ya Umoja wa Afrika (AU) pamoja na mifumo ya Kiafrika
kama vielelezo. Mapendekezo yanayotolewa kwenye taarifa ya AMB hatimaye
yanajumuishwa kwenye tathmini nyinginezo zilizofanyika kwenye nchi zipatazo
20 zenye ofisi za FES Kusini mwa Bara la Afrika, na kujumuishwa pia kwenye
jitihada mbalimbali za ushawishi kuhusu vyombo vya habari unaofanywa na
taasisi nyingine za vyombo vya habari katika nchi husika kama vile MISA.
Mbinu na mfumo wa utoaji alama
Kila baada ya miaka mitatu hadi minne, jopo la wataalam kati ya 10 na 12 lenye
kujumuisha angalau wanahabari watano na wawakilishi watano wa asasi za
kiraia hukutana kwa lengo la kutathmini hali ya vyombo vya habari katika nchi
zao wenyewe. Kwa muda wa siku moja na nusu hivi, jopo hilo hujadili mazingira
ya vyombo vya habari kwa kuzingatia vigezo 39 ambavyo hutumika kama adidu
za rejea. Mjadala na utoaji wa alama hujadiliwa pamoja mshauri elekezi ambaye
pia huhariri taarifa ya AMB.
Baada ya kujadili kigezo kimoja, wanajopo huweka alama zao kwenye kigezo
husika ambapo huridhiwa kwa kura ya pamoja kwa mujibu wa kielelezo
kifuatacho:

2

1

Nchi inakidhi kiashiria

2

Nchi inakidhi vipengele vichache tu vya kiashiria

3

Nchi inakidhi vipengele kadhaa vya kiashiria

4

Nchi inakidhi vipengele vingi vya kiashiria

5

Nchi inakidhi vipengele vyote vya kiashiria

KIPIMO CHA VYOMBO VYA HABARI BARANI AFRIKA TANZANIA 2019

Select target paragraph3