ENEO LA 3

Mshiriki mmoja alielezea jinsi ambavyo kipande maarufu kilitoweka kwenye
taarifa ya habari:
TBC ilikuwa na kipande cha makala kilichokuwa kinaitwa In Between
the News, ambapo mtaalam au mchambuzi alikuwa anaalikwa kutoa
maoni kuhusu matukio muhimu kwenye taarifa ya habari. Muda fulani,
Rais aliwasamehe watu ambao walikuwa wametumia fedha za umma
vibaya. Kabla ya kuwa hewani, aliambiwa, “Leo inabidi uongee vizuri
kuhusu serikali na kuipongeza serikali kwa kufanya kitu kizuri”. Lakini
alipokuwa hewani, alisema ilikuwa ni makosa kwa msamaha wa Rais
kutolewa kabla ya wahusika kushtakiwa mahakamani ili kuwatia hatiani
au kuwaachia huru. Kuanzia siku hiyo, kipindi cha In Between the News
kilifutwa.
Ili kuendelea kuwa hewani, TBC ina msururu wa matangazo ya tamthiliya,
orodha ya miziki na vipindi vinavyoelezea ‘namna ya kuwa mzalendo na raia
mwema au kuwa mke mzuri’.

Alama:
Alama za mshiriki mmoja mmoja:
1

46

Nchi inakidhi kiashiria

2

Nchi inakidhi vipengele vichache tu vya kiashiria

3

Nchi inakidhi vipengele kadhaa vya kiashiria

4

Nchi inakidhi vipengele vingi vya kiashiria

5

Nchi inakidhi vipengele vyote vya kiashiria

✓

✓

✓✓✓✓✓✓✓✓

✓

Wastani wa alama:
Alama ya miaka iliyopita:

2.4
2006: n/a; 2008: n/a; 2010: n/a; 2012: n/a; 2015: 2.6

Jumla ya alama kwenye sekta 3:

2.0

KIPIMO CHA VYOMBO VYA HABARI BARANI AFRIKA TANZANIA 2019

✓

Select target paragraph3