ENEO LA 2

2.13 Ukubwa wa soko la utangazaji unawezesha
uwepo wa mchanganyiko wa vyanzo vya habari
Makampuni ya habari yanalalamika kwamba hawapati matangazo ya biashara
ya kutosha ili kuwezesha uendeshaji. Washiriki waliona kwamba, hakika, soko la
matangazo ya biashara limedorora kwa miaka mingi na kubakia na watangazaji
biashara wachache tu; hasa mashirika ya mawasiliano ya simu, viwanda vya bia na
mabenki. Kwenye mijadala, ilionekana kwamba sababu kuu mbili zimebadilisha
sura ya soko la matangazo ya biashara Tanzania. Mosi, serikali inadhibiti sehemu
kubwa ya matumizi kwenye matangazo ambayo yanarushwa kwa kuvipendelea
vyombo vinavyomilikiwa na serikali na vile vya binafsi vyenye kuelemea upande
wa serikali. Pili, watoaji wakubwa wa matangazo ya biashara wa zamani sasa
wanamiliki vyombo vyao wenyewe vya habari. Hali hii si tu kwamba imebana
soko la matangazo ya biashara, lakini pia imeondoa usawa kwenye mgao wa
mapato yatokanayo na matangazo ya biashara kwenye tasnia nzima.
Mmoja wa washiriki alisema vyombo vya habari pia havikuwa na uwezo wa
kuvutia matangazo, akieleza kwamba:
Biashara mpya zinaanzishwa kila siku na zinahitaji kutangazwa. Tatizo
ni kwamba vyombo vya habari vinawakimbilia watoaji matangazo wale
wale. Kama wanatarajia kupata matangazo kutoka serikalini tu na
kwenye makampuni machache, basi wanaweza wasipate ya kutosha.
Redio za kijamii wanalijua hili na ndo maana wanaenda kwenye sekta
isiyo rasmi. Tunatakiwa tuelewe kwamba mambo ni magumu na kuacha
kubagua.
Ushindani kutoka kwa majukwaa mbadala kama vile mitandao ya kijamii
pia umeongezeka. Watu wengi na wafanyabiashara wadogo wameugezia
matangazo ya biashara kwenye mtandao. ‘Changamoto kwa vyombo vya habari
ni kwenda na mabadiliko haya.’

Alama:
Alama za mshiriki mmoja mmoja:

39

1

Nchi inakidhi kiashiria

2

Nchi inakidhi vipengele vichache tu vya kiashiria

3

Nchi inakidhi vipengele kadhaa vya kiashiria

4

Nchi inakidhi vipengele vingi vya kiashiria

5

Nchi inakidhi vipengele vyote vya kiashiria

✓✓
✓

✓

✓

✓✓✓✓

✓

✓

Wastani wa alama:
Alama ya miaka iliyopita:

3.0
2006: 2.1; 2008: 1.9; 2010: 2; 2012: 2.5; 2015: 2.2

Jumla ya alama kwenye sekta 2:

2.7

KIPIMO CHA VYOMBO VYA HABARI BARANI AFRIKA TANZANIA 2019

✓

Select target paragraph3