ENEO LA 1

wa kisiasa na kijamii. Kwa mujibu wa washiriki, panapokuwa na majadiliano,
mawazo ambayo hayaoani na mtizamo wa serikali hayazingatiwi. Katika hali ya
kupindukia, serikali hutumia makundi na watu binafsi nje ya mfumo rasmi wa
kisheria kushadidia msimamo wa serikali wakati wa vikao vya majadiliano- na
hivyo kuzima sauti za watu wenye mawazo kinzani.
Utamaduni huu wa utungaji wa sheria unadhihirika pia kwenye sheria
zinazohusu vyombo vya habari. Ili kuzuia mijadala (hata ndani ya bunge), mara
nyingi mamlaka hutumia nyenzo inayoitwa ‘hati ya dharura’, ambayo hutumiwa
kuharakisha kupitisha sheria kwa kupunguza ngazi za uchambuzi ambazo
mswada unatakiwa kupitia kwenye bunge. Miaka michache iliyopita, sheria
mbili zenye athari za moja kwa moja kwa vyombo vya habari zimepitishwa kwa
kutumia mtindo huu. Sheria hizo ni ile ya Makosa ya Mtandaoni na ile Sheria ya
Takwimu.
Washiriki walitabanaisha kwamba wakati mwingine majadiliano husababisha
kuwepo kwa sheria mbaya zaidi za vyombo vya habari- watetezi wa vyombo
vya habari walishindwa kuzuia kutungwa kwa Sheria ya Vyombo vya Habari na
inawezekana wakawa wamesaidia kuharakisha matumizi yake. Hatua dhahiri
inayoonesha kutoheshimiwa kwa madai yao, ni kwamba Sheria ya Vyombo vya
Habari ilitiwa sahihi kuwa sheria kamili siku moja baada ya kikao kati ya makundi
ya watetezi wa vyombo vya habari na mamlaka husika, ambapo watetezi wa
vyombo vya habari walikuwa wametoa mapingamizi dhidi ya sheria hiyo.
Ushawishi wa umma kwenye mchakato wa kutunga sheria ulizaa matunda
kwenye matukio machache. Sheria ya Upatikanaji wa Habari, mathalan,
ilisimamishwa kwa mwaka mmoja kutokana na malalamiko ya wananchi.
Washiriki walisema kwamba washawishi wa vyombo vya habari walifanikiwa
kuondoa kifungu ambacho kinapiga marufuku kutumia taarifa zilizopatikana
kupitia ombi la FOI kwa umma. Kifungu hiki kilirithiwa na kifungu kingine chenye
unafuu zaidi ingawa bado kandamizi, ambacho kiliharamisha kubadili maudhui
ya habari zilizopatikana kutoka kwa ombi la FOI.

Alama:
Alama za mshiriki mmoja mmoja:

27

1

Nchi inakidhi kiashiria

2

Nchi inakidhi vipengele vichache tu vya kiashiria

3

Nchi inakidhi vipengele kadhaa vya kiashiria

4

Nchi inakidhi vipengele vingi vya kiashiria

5

Nchi inakidhi vipengele vyote vya kiashiria

✓✓

✓
✓

✓

✓✓
✓

✓

✓✓✓

Wastani wa alama:
Alama ya miaka iliyopita:

2.0
2006: n/a; 2008: n/a; 2010: 2.6; 2012: 3.8; 2015: 1.7

Jumla ya alama kwenye sekta 1:

2.2

KIPIMO CHA VYOMBO VYA HABARI BARANI AFRIKA TANZANIA 2019

Select target paragraph3