NINI KIFANYIKE

1.

Miaka mitatu hadi minne iliyopita, kulikuwa na
mabadiliko gani kwenye mazingira ya vyombo vya
habari?
Mabadiliko Chanya
•

Kuongezeka kwa idadi ya vyombo vya habari kulikoambatana na kupanuka
kwa mitandao ya kijamii kumezuia jaribio la mamlaka kufunga majukwaa
ya kujieleza kwa uhuru.

•

Fursa zaidi za mafunzo yanayojumuisha wadau wapya zimeibuka katika
kipindi cha miaka michache iliyopita, na hivyo kuwapa waandishi wa habari
wigo mpana zaidi wa kufanya maamuzi.

•

Vyama vya waandishi wa habari vimekuwa imara zaidi katika kuvilinda
vyombo vya habari dhidi ya madhila mbalimbali ya vyombo vya habari na
uhuru wa uandishi wa habari.

Mabadiliko Hasi

2.

61

•

Fursa za kisiasa na vyombo vya habari zinasinyaa, hasa kutokana na
kuanzishwa kwa sheria kandamizi tangu mwaka 2015.

•

Ongezeko la matumizi ya wataalam wapotoshaji kwenye mitandao ya
kijamii ili kudhibiti uhuru wa kujieleza kumesababisha athari mbaya, na
hivyo kuzuia uhuru wa kujieleza.

•

Wanawake wamezidi kuwa na taswira hasi mbele ya viongozi waandamizi
wa serikali na kwenye vyombo vya habari.

•

Imekuwa ni vigumu sana kupata vyanzo vya habari, hususan kutoka kwenye
ofisi za umma.

Ni jitihada gani zinahitajika katika kipindi cha
miaka mitatu hadi minne ijayo?
•

Kuna haja ya kuwa na mikakati ya kisheria na ushawishi dhidi ya sheria
kandamizi, na harakati hizi zinaweza kuongozwa na CORI.

•

Kuna haja ya kuongeza mafunzo kuhusu usalama wa vyombo vya habari
na mchanganyiko, na harakati hizi zinaweza kuongozwa na UNESCO/TMF/
MCT/THRDC.

•

Kuna haja ya kundelea kufanya ushawishi kwa ajili ya kufufua vyama vya
wafanyakazi wa vyombo vya habari na kuungana na Shirikisho la Kimataifa
la Waandishi wa Habari.

•

Kuna haja ya makampuni ya vyombo vya habari kufanya jitihada za maksudi
kwa minajili ya kurasimisha mafunzo na kutengeneza fursa zaidi za mafunzo
kwenye maudhui yanayowalenga watu wenye ulemavu, jinsia na haki za
binadamu.

KIPIMO CHA VYOMBO VYA HABARI BARANI AFRIKA TANZANIA 2019

Select target paragraph3